Monday, 11 July 2022

Usajili wa wachezaji soka Ulaya

Hapa utaona dondoo za usajili kutoka  maeneo mbalimbali Ulaya.


Arsenal inachuana na Manchester United katika harakati za kumsajili kiungo wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante (31).



Kiungo wa Barcelona na Hispania Sergio Busquets (33) anasakwa na vilabu kadhaa vya ligi ya Marekani MLS ili kujiunga navyo msimu ujao.


Chelsea inataka £7m kutoka kwa Barcelona kwa ajili ya mlinzi wake mhispania Cesar Azpilicueta (32)  ambaye ameshakubaliana  kuhusu maslahi binafsi na klabu hiyo ya Catalan.


Arsenal na Newcastle zinamtaka kiungo mshambuliaji wa Lyon na Brazil Lucas Paqueta lakini ada ya 65m euros inayotakiwa na wafaransa hao kwa ajili ya nyota huyo mwenye miaka (24).

Arsenal iko kwenye mazungumzo na Benfica baada ya kupeleka ofa ya £6.4m kwa ajili ya kumsajili beki wa kushoto mhispania Alex Grimaldo (26).



Chelsea wanajiandaa kukubaliana na ada wanayotaka Napoli ya £34m kwa ajili ya mlinzi wake wa kati raia wa Senegal Kalidou Koulibaly (31).


Bayern Munich inamsaka mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane (28) kama mbadala wa Robert Lewandowski (33) kutoka Poland anayetaka kuachana na mabingwa hao wa Bundesliga msimu huu.


Chelsea na Paris St-Germain nazo zitaingia kwenye mbio za kutaka saini ya  Lewandowski kama itashindikana kujiunga na Barcelona.


Barcelona wanaamini watamsajili kiungo mreno Bernardo Silva (27) kutoka Manchester City.


Labels:

Sunday, 10 July 2022

Akpan asajiliwa Simba Sc

Kiungo wa katikati ya dimba mwenye uwezo mkubwa wa kuhimili mechi za aina zote. 

Victor Akpan ni 𝗠𝗡𝗬𝗔𝗠𝗔 🦁 #Akpan #NguvuMoja

Labels:

Dispatch clerk II Simba Cement Plc New Vacancy

Simba Cement PLC (the Tanga Cement Company Limited) has the capacity to produce more than 1.25 million tonnes of Simba cement and more than 1.25 million tonnes of clinker. 

The primary raw material, limestone, is located at the plant site. The Company completed second largest expansion project by installing kiln number two. The first expansion project by the company involved installation of cement mill number two and packer III. Tanga Cement Company’s manufacturing facilities are ISO 9001: certified. Simba cement products are produced in accordance with Tanzania Cement Standard TZS 721-1: which is equivalent to East African standard for cement EAS 18-1: and European Standard for cement EN 197-1. Tanga Cement PLC is located about 15 kilometre from Tanga city centre. The company is incorporated in Tanzania under the Tanzanian companies Act 2002 as a public company limited by shares. Our Vision. To be the East Africa’s preferred cement manufacturer and distributor. Our Mission. To develop, produce and distribute consistently high quality cement and related products and services in a sustainable manner to satisfy our customers’ expectations.


The company is looking to hire individuals to fill a new vacant position.  Read full details from the PDF Document below.


CLICK HERE


Labels:

Saturday, 9 July 2022

Kyombo rasmi atua Simba

 HATIMAYE, Simba imepata saini ya aliyekuwa mshambuliaji wa Mbeya Kwanza, Habib Kyombo kwa mkataba wa miaka miwili baada ya kutokea sintofahamu hapo awali.

Awali nyota huyo alidaiwa kusaini timu mbili tofauti akianza na wageni wa Ligi Kuu Bara Singida Big Stars kisha kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pande mbili baada ya kukubali dili jipya la kujiunga na Simba.


Wakati akiitumikia Mbeya Kwanza katika msimu ulioisha Juni 29, mwaka huu staa huyo alifunga mabao sita ya Ligi Kuu Bara katika mechi 15 alizocheza na kikosi hicho ambacho  kimeshuka daraja baada ya matokeo mabovu.


Huu ni usajili wa kwanza Simba kwa wachezaji wazawa msimu huu baada ya ule wa Moses Phiri raia wa Zambia aliyejiunga na miamba hiyo Juni 15 akitokea klabu ya Zanaco ya huko nchini kwao Zambia.


Mbali na Usajili huo kuna nyota wengine wanaosadikika wamejiunga na miamba hiyo ni Victor Akpan kutoka Coastal Union, Cesar Manzoki (Vipers FC), Nelson Okwa (Rivers United) na Augustine Okrah aliyetokea Asante Kotoko.


Labels:

Friday, 8 July 2022

Sepp Blatter na Michel Platini wafutiwa mashtaka ya ulaghai na mahakama ya Uswizi

Sepp Blatter na Michel Platini wafutiwa mashtaka ya ulaghai na mahakama ya Uswizi.

  • Wawili hao waliachiliwa huru kwa shtuma ya kufanya malipo ya faranga za Uswizi milioni 2 yaliyofanywa mwaka 2011.
  • Malipo yaliyofanywa kwa Platini kwa huduma za ushauri za Fifa.


Sepp Blatter na Michel Platini wamefutiwa mashtaka ya ulaghai katika mahakama ya Uswizi. 


Wanaume hao wawili, waliokuwa miongoni mwa vigogo wa soka, waliachiliwa huru kwa kupanga malipo ya faranga milioni mbili za Uswizi (£1.7m) kinyume cha sheria mwaka 2011. Wakati huo, Platini alikuwa rais wa Uefa na makamu wa rais wa Fifa na alitarajiwa kumrithi Blatter kama rais wa Fifa, shirikisho la soka duniani.


Malipo kwa Platini kwa huduma za ushauri katika muhula wa kwanza wa Blatter kama rais, kuanzia 1998 hadi 2002, yaliidhinishwa na Blatter Januari 2011 lakini yakaishia kumaliza kazi za wanaume katika soka.


 Waendesha mashtaka wa Uswizi walikuwa wameiambia mahakama huko Bellinzona kwamba "ilifanyika bila msingi wa kisheria" na "ilimtajirisha Platini isivyo halali" lakini hakimu katika kesi yao aliwakuta hawana hatia. Platini sasa atarejeshewa CHF 2m yake. 


Kamati ya maadili ya Fifa ilikuwa imewapiga marufuku kujihusisha na soka na kuwaondoa madarakani, na Blatter na Platini walipeleka kesi zao kwa kamati ya rufaa ya Fifa bila mafanikio na baadaye katika rufaa tofauti kwa mahakama ya usuluhishi wa masuala ya michezo.


#soma zaidi HAPA


Labels:

CAG Kichere naye alia na Tume ya uchaguzi ifumuliwe

Aungana na viongozi wengine, wakiwemo wastaafu, wanaotaka tume ya uchaguzi iwe na watendaji walio huru ili iweze kuaminika.

Dar es Salaam. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere ameishauri Serikali kuipa nguvu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuajiri watumishi wake watakaoweza kusimamia uchaguzi kwa haki badala ya kuendelea kutegemea waliopo kwenye mfumo wa Serikali.

Mei 10, 2019, Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya kubatilisha vifungu vya 7(1) na 7(3) vya sheria ya uchaguzi vinavyowapa mamlaka wakurugenzi wa miji, wilaya, manispaa na majiji kuwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye maeneo yao.

Shauri hilo lilifunguliwa na mwanaharakati wa Katiba, Bob Wangwe akishirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

Hata hivyo, Serikali ilikata rufaa kuipinga hukumu huyo na baadaye Oktoba 2019 Mahakama ya Rufani ikabatilisha uamuzi na hivyo kuruhusu wakurugenzi waendelee kusimamia uchaguzi.

#soma zaidi HAPA











Labels:

Thursday, 7 July 2022

Data Entry Officer Job Opportunity at Norwegian Refugee Council

Job title: Data Entry Officer

Posting Date: 06/07/2022, 15:20

Apply Before: 18/07/2022, 15:20

Degree Level: Three Years College


Job Description

All NRC employees are expected to work in accordance with the organization’s core values: dedication, innovation, inclusivity and accountability. These attitudes and believes shall guide our actions and relationships.


Responsibilities


  • Develop data collection methods and tools to support programs in needs assessment, baseline assessment, output and outcome monitoring and evaluation of the on-going projects.
  • Data management, entry and analysis.
  • Prepare and submit weekly and monthly reports
  • Ensure proper filing of project documents and reports
  • Conduct routine monitoring and follow-up of project activities
  • Other activities agreed and discussed with supervisor
  • Responsible for managing, recording, sharing, following up and consolidating WASH committee feedback about NRC’s WASH interventions
  • Work closely with the program teams, M&E.
  • Responsible for data collection, entry and management.


Qualifications

  • University degree in Social Sciences, Statistics, Information Systems Management, or related qualification.
  • Additional training in data management and information system is an added advantage.
  • At least 3 years of experience in an NGO preferably in humanitarian setting.
  • Good interpersonal skills and ability to collaborate with multiple stakeholders, mainly communities effectively.
  • Ability to receive and handle confidential and sensitive information (highly approachable, trustworthy and confidential)
  • Computer skills, including MS Office (Word, Excel)
  • Fluency in English, both written and verbal
  • Working with people
  • Communicate with impact and respect
  • Ability to work under pressure, independently and with limited supervision
  • Patient, flexible and creative


Duty station: Kibondo-Nduta


Department: WASH-Kibondo. 

Duration and type of contract: 6 months – with possible extension.


Click here to APPLY










Labels:

Ukweli usiopingika alio uandika Roma

Jana Nilitafakari Nikagundua Age Yangu Na Kaka Zangu Wengine Imeenda Sana.



Tunazeeka Sasa, Niliona  Mabantu Kwenye Interview Wanamuita Country Boi Kaka, Halafu Unakuta Mimi Country Ananiita Kaka Pia, Means Mabantu Wataniitaje Mm? Mm Namuita FID Kaka, Mabantu Watamuitaje FID? #Tunazeeka

Labels:

Taarifa kwa UMMA kuhusu ajira ya Sensa

Taarifa kwa umma kuhusu sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.

Ofisi ya Taifa ya Takwimu imetoa tangazo hili na kulitolea ufafanuzi. Soma zaidi HAPA


Pia Kamisaa wa Sensa Anna Makinda, amesema baadhi ya Watanzania wanapenda uongo kutokana na maneno ya uzushi yanayozagaa mitandaoni kwamba majina ya wasimamizi wa Sensa hayatoki kwa sababu wameweka watoto wao, na kusema majina yakitoka waombaji wote wenye sifa watachukuliwa.


Labels:

Nandy kuja na project mpya

Msanii mwanadada wa kizazi kipya Nandy anatarajia kuachia project yake mpya hivi karibuni.

Baada ya kupost twitter statement hii "tutoe project mpya nimewamiss", wadau walitiririka na kusema project wanaoisubiri ni kwa sasa kutoka kwake ni ndoa.

Unaweza kusoma zaidi comments Bonyeza







Labels:

Timu ya taifa Ghana yafanya usajili

Tariq Lamptey abadili utaifa kutoka Uingereza hadi Ghana.

Chama cha Soka cha Ghana kilithibitisha kuwa beki huyo wa pembeni wa Brighton, ambaye aliiwakilisha Uingereza katika mechi tofauti za vijana na kucheza mara mbili kwa Vijana wa U-21, aliamua kuchezea Black Stars.


Atakuwepo kwenye mchujo kuelekea Kombe la Dunia nchini Qatar, ambapo Ghana itamenyana na Korea Kusini, Ureno na Uruguay katika Kundi D.


"Siku zote tumeshikilia kuwa hatutajiwekea kikomo kwa kikundi kidogo tu cha wachezaji lakini tutasaka vipaji vya juu kote ulimwenguni ambao wako tayari kujitolea kwa ajili ya taifa na kutupeleka kwenye ngazi nyingine," taarifa kutoka Chama cha Soka Ghana ilisema hivyo.


Mchezaji mwingine alie amua kulitumikia taifa hilo ni Inaki Williams anaekipiga kunako Athletic Bilbao inayocheza ligi kuu ya Uhispania (LaLiga).

Labels:

DC Kigoma aagiza uchunguzi ujenzi wa Zahanati

Mkuu wa wilaya ya Kigoma Ester Mahawe ameagiza mamlaka ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Kigoma, kufanya uchunguzi katika mradi wa Zahanati ya kijiji cha Samwa kata ya Kidakhwe wilayani Kigoma kufuatia mradi huo kutumia gharama kubwa na kupitiliza muda wa utekelezaji.




Agizo hilo amelitoa baada ya kamati ya siasa chama cha mapinduzi wilaya ya kigoma kufanya ziara kijijini hapo, ambapo wananchi wamelalamika mradi huo kushidwa kukamilika kwa wakati licha ya kuendelea kukosa huduma za matibabu karibu.

Awali kaimu Mganga Mkuu wa wilaya ya Kigoma Erasto Kitabi alieleza mradi huo kusuasua kutokana na mkandarasi anayesimamia kutokuwa na uhusiano mzuri na kamati ya ujenzi licha ya kupewa fedha zote za mradi kiasi cha shilingi milioni 70.

#source Eatv










Labels:

Christian Eriksen kutua Man United

Mikataba sasa iko tayari kwa Christian Eriksen kusaini na Manchester Utd, kinachosubiriwa ni vipimo tu ndipo itakamilika.

Mkataba wa miaka mitatu umethibitishwa, Eriksen ndiye atakayesajiliwa na United baada ya Tyrell Malacia.

#source Twitter












Labels:

Waziri Mkuu Uingereza ajiuzulu

 Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson amejiuzulu nafasi ya kiongozi wa Chama cha Conservative.


London. Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson amejiuzulu nafasi ya kiongozi wa Chama cha Conservative.


Boris amejiuzulu nafasi hiyo leo Alhamisi Julai 7, 2022 lakini bado atabaki kuwa Waziri Mkuu mapaka chama hicho kitakapopata kiongozi mpya mwezi Oktoba.


Katika hotuba yake, Boris amesema “Nina huzuni kuacha kazi bora zaidi duniani. Ninataka ujue jinsi ninavyohuzunishwa na kuacha kazi bora zaidi duniani,’’


"Nimekubaliana na Sir Graham Brady, mwenyekiti wa wabunge wetu wa viti maalum, kwamba mchakato wa kumchagua kiongozi mpya uanze sasa na ratiba itatangazwa wiki ijayo. Na leo nimeteua Baraza la Mawaziri kuhudumu, pia nitaendelea kuongoza hadi kiongozi mpya atakapochaguliwa.’’


 Amejiuzulu baada ya kuhudumu katika wadhifa huo chini ya miaka mitatu, licha ya kupata ushindi mkubwa katika uchaguzi wa 2019. 


Kinachofuatia baada ya kiongozi huyo wa Conservative kujiuzulu, uchaguzi wa kiongozi mpya wa chama unaanzishwa ambapo chini ya sheria za sasa, wagombea wanahitaji kuungwa mkono na wabunge wanane wa chama hicho ili kuwania. 


#Soma zaidi HAPA










Labels:

Raheem Sterling anakaribia kuhamia Chelsea


Chelsea watawasiliana moja kwa moja na Manchester City leo ili kukamilisha dili la Raheem Sterling. Ada karibu ikubaliwe pauni milioni 45 za uhakika pamoja na nyongeza, sawa na Gabriel Jesus kwa Arsenal. 


Masharti ya kibinafsi yalikubaliwa kikamilifu, Tuchel tayari alikuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na Sterling. 

#source Twitter

Labels: