Monday, 11 July 2022

Usajili wa wachezaji soka Ulaya

Hapa utaona dondoo za usajili kutoka  maeneo mbalimbali Ulaya.


Arsenal inachuana na Manchester United katika harakati za kumsajili kiungo wa Chelsea na Ufaransa N'Golo Kante (31).



Kiungo wa Barcelona na Hispania Sergio Busquets (33) anasakwa na vilabu kadhaa vya ligi ya Marekani MLS ili kujiunga navyo msimu ujao.


Chelsea inataka £7m kutoka kwa Barcelona kwa ajili ya mlinzi wake mhispania Cesar Azpilicueta (32)  ambaye ameshakubaliana  kuhusu maslahi binafsi na klabu hiyo ya Catalan.


Arsenal na Newcastle zinamtaka kiungo mshambuliaji wa Lyon na Brazil Lucas Paqueta lakini ada ya 65m euros inayotakiwa na wafaransa hao kwa ajili ya nyota huyo mwenye miaka (24).

Arsenal iko kwenye mazungumzo na Benfica baada ya kupeleka ofa ya £6.4m kwa ajili ya kumsajili beki wa kushoto mhispania Alex Grimaldo (26).



Chelsea wanajiandaa kukubaliana na ada wanayotaka Napoli ya £34m kwa ajili ya mlinzi wake wa kati raia wa Senegal Kalidou Koulibaly (31).


Bayern Munich inamsaka mshambuliaji wa Tottenham na England Harry Kane (28) kama mbadala wa Robert Lewandowski (33) kutoka Poland anayetaka kuachana na mabingwa hao wa Bundesliga msimu huu.


Chelsea na Paris St-Germain nazo zitaingia kwenye mbio za kutaka saini ya  Lewandowski kama itashindikana kujiunga na Barcelona.


Barcelona wanaamini watamsajili kiungo mreno Bernardo Silva (27) kutoka Manchester City.


Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home