Friday, 8 July 2022

CAG Kichere naye alia na Tume ya uchaguzi ifumuliwe

Aungana na viongozi wengine, wakiwemo wastaafu, wanaotaka tume ya uchaguzi iwe na watendaji walio huru ili iweze kuaminika.

Dar es Salaam. Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere ameishauri Serikali kuipa nguvu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuajiri watumishi wake watakaoweza kusimamia uchaguzi kwa haki badala ya kuendelea kutegemea waliopo kwenye mfumo wa Serikali.

Mei 10, 2019, Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya kubatilisha vifungu vya 7(1) na 7(3) vya sheria ya uchaguzi vinavyowapa mamlaka wakurugenzi wa miji, wilaya, manispaa na majiji kuwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye maeneo yao.

Shauri hilo lilifunguliwa na mwanaharakati wa Katiba, Bob Wangwe akishirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC).

Hata hivyo, Serikali ilikata rufaa kuipinga hukumu huyo na baadaye Oktoba 2019 Mahakama ya Rufani ikabatilisha uamuzi na hivyo kuruhusu wakurugenzi waendelee kusimamia uchaguzi.

#soma zaidi HAPA











Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home