Thursday, 7 July 2022

Timu ya taifa Ghana yafanya usajili

Tariq Lamptey abadili utaifa kutoka Uingereza hadi Ghana.

Chama cha Soka cha Ghana kilithibitisha kuwa beki huyo wa pembeni wa Brighton, ambaye aliiwakilisha Uingereza katika mechi tofauti za vijana na kucheza mara mbili kwa Vijana wa U-21, aliamua kuchezea Black Stars.


Atakuwepo kwenye mchujo kuelekea Kombe la Dunia nchini Qatar, ambapo Ghana itamenyana na Korea Kusini, Ureno na Uruguay katika Kundi D.


"Siku zote tumeshikilia kuwa hatutajiwekea kikomo kwa kikundi kidogo tu cha wachezaji lakini tutasaka vipaji vya juu kote ulimwenguni ambao wako tayari kujitolea kwa ajili ya taifa na kutupeleka kwenye ngazi nyingine," taarifa kutoka Chama cha Soka Ghana ilisema hivyo.


Mchezaji mwingine alie amua kulitumikia taifa hilo ni Inaki Williams anaekipiga kunako Athletic Bilbao inayocheza ligi kuu ya Uhispania (LaLiga).

Labels:

0 Comments:

Post a Comment

Subscribe to Post Comments [Atom]

<< Home