Benki Kuu Yapunguza Riba kwa Mabenki ya Biashara
Benki kuu Tanzania imepunguza kiwango cha riba kwa mabenki ya biashara kufikia asilimia 11.
![]() |
Katika hatua nyingine, riba za dhamana za serikali zimepunguzwa kufikia wastani wa asilimia sita, hatua hiyo itapunguza mabenki kufanya biashara na serikali na badala yake kuwakopesha watu wa kawaida kutokana na faida ya kuikopesha serikali kuwa ndogo sana ukilinganisha na kukopesha watu wa kawaida.
Naibu gavana wa Benki kuu, Dr. Kibesse amesema benki kuu imekuwa ikichukua hatua hizo ili kuwawezesha wananchi wamudu kukopa ndio maana kiwango cha riba kimekuwa kikishuka.
Akiwa kwenye kikao na wafanyabiashara Ikulu Juzi, Rais Magufuli alielezea azma ya serikali kufanya fedha yake kuwa ngumu kwa mabenki ili warudi kwa wananchi ikiwemo kupunguza kutoa hati fungani za serikali kwa mabenki
Labels: ECONOMY
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home