Rolihlahla Mandela
Mandela alisoma katika Chuo Kikuu cha Fort Hare na Chuo Kikuu cha Witwatersrand. Akawa mwanasheria mwaka 1942. Mwaka 1944, alijiunga na Chama cha ANC, chama kilichodhamiria kuutokomeza utawala wa makaburu weupe pekee. Mwaka 1960, Chama tawala cha makaburu kilikipiga marufuku cha cha ANC na kuwashitaki viongozi wake kwa kosa la uhaini, lakini Mandela aliachiwa huru.
MAJINA YA UTANI: Madiba, Black Pimpernel
MAHALI ALIKOZALIWA: Mveso, Transkei, South Africa
KAZI: Mwanaharakati, Kiongozi wa dunia
TAREHE YA KUZALIWA: Julai 18, 1918
TAREHE YA KUFA: DESEMBA 05, 2013
MAHALI ALIKOFIA: Johannesburg, South Africa
ELIMU: Taasisi ya Clarkebury, Chuo cha Wesleyan, Chuo Kikuu Kishiriki cha Fort Hare, Chuo Kikuu cha London, Chuo Kikuu cha Witwatersrand, Johannesburg.
![]() |
Rolihlahla Mandela |
KUFUNGWA GEREZANI
Akiendeleza harakati zake za kupambana na makaburu, Mandela alikamatwa, akatiwa hatiani na kuhukumiwa kifungo cha maisha gerezani kuanzia mwaka 1964 hadi 1990, ambapo maisha yake kama kiongozi wa harakati za kupambana na ubaguzi wa rangi yakajulikana dunia nzima. Kama mfungwa wa dhamiri, Mandela mara kwa mara alikataa kuachiwa kwa masharti.
KUACHIWA HURU
Mwaka 1990, akiwa amekaa jela kwa miaka 26 na akiwa na umri wa miaka 71, iliachiwa huru bila masharti yoyote baada ya utawala wa kibaguzi kushinikizwa na jumuiya ya kimataifa. Mwaka 1993, Nelson Mandela alishinda Tuzo ya Nobel kwa harakati zake za kisiasa.
![]() |
The late Rolihlahla Mandela with his family members |
Labels: Heroes
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home