Tetesi za Soka Ulaya Jumatatu ya Leo
![]() |
Meneja wa Chelsea Antonio Conte |
Manchester City wanampango wa kumsajili kiungo wa kati wa Chelsea Eden Hazard 27, kwa mkataba wa £100m baada ya meneja Pep Guardiola kumuweka mchezaji huyo kuwa kiungo muhimu anayemlenga wakati wa uhamisho.(Star)
Klabu ya Utaliano ya AC Milan imempatia kiungo wa kati wa Manchester United Marouane Fellaini 30, mkataba wa miaka mitatu huku kiungo huyo raia wa Ubelgiji kuwa huru kwa uhamisho wa bure katika majira ya joto. (Times - subscription required)
Beki wa Tottenham,Toby Alderweireld 29, ni miongoni mwa wanaotarajiwa kuuzwa na klabu hiyo kwenda Manchester United wakati wa uhamisho wa majira ya joto. (Mirror)
West Ham inaamini kumteuwa Manuel Pellegrini kama meneja wao mpya wiki hii- ambayo itaipatia nafasi nzuri ya kumsajili kiungo wa kati Yaya Toure, 35, aliyeiaga Manchester City. (Telegraph)
Meneja wa Chelsea Antonio Conte anatarajiwa kuiaga Chelsea kwa saa 48 zijazo - huku meneja wa zamani wa Barcelona Luis Enrique anatarajiwa kuchukua nafasi hiyo. (Express)
![]() |
Kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere |
Kiungo wa kati wa Arsenal Jack Wilshere, 26 yuko tayari kutia saini mkataba wa miaka mitatu aliyopewa na Arsenal, licha ya kupata mapendekezo bora kutoka Everton na Wolves. (Mirror)
Manchester United imekubaliana katika hatua za kwanza na kiungo wa kati kutoka Brazil Talisca, 24 ambaye amekuwa kwenye mkopo na Besiktas kutoka Benfica. (Star)
Kocha wa zamani wa Paris St-Germain Unai Emery ni miongoni mwa makocha wanaowania kukinoa kikosi cha Arsenal msimu ujao wa ligi kuu huku Mikel Arteta akiwa bado ni mmoja wa makocha anaetazamiwa kuchukua nafasi ya Arsene Wenger. (Dail Mail)
![]() |
Mlinda lango kutoka Ubelgiji Thibaut Courtois |
Mlinda lango kutoka Ubelgiji Thibaut Courtois 26, ametishia kuihama Chelsea iwapo klabu hiyo haitatumia pesa zake kama klabu za ''Manchester United na City'' msimu huu wa joto. (Sun)
Mazungumzo ya Napoli na meneja wao Maurizio Sarri yametibuka kutokana na matamanio ya meneja huyo kutaka kuhamia Chelsea. (Mirror)
Mhispania Santi Cazorla 33, amepewa nafasi ya kujiunga na klabu yake ya zamani ya Villarreal kuelekea kumalizika kwa mkataba wake na Arsenal. (Evening Standard)
![]() |
Kiungo wa kati wa Ac Milan Suso |
Kiungo wa kati wa Ac Milan Suso 24, anatarajiwa kurudi Liverpool lakini si kwa mara moja kwa siku zijazo. (Liverpool Echo)
Beki Partick Thistle Niall Keown 23, anatarajiwa kubadili majukumu yake kutoka Republic hadi Kaskazini mwa Ireland - na meneja Michael O'Neill anataka kumsajili kiungo wa kati wa Klabu ya QPR Sean Goss 22, kwa mkopo. (Daily Record)
![]() |
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho |
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amefuta akaunti yake ya Instagram kutokana na matusi ambayo aliyoyapata baada ya mashetani hao wekundu kushindwa kwenye fainali ya kuwania kombe la FA dhidi ya Chelsea. (Sun)
Labels: Sports
0 Comments:
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
<< Home